- Kuchapa ramani katika rangi nyingi au moja hadi ukubwa wa 30" X 40"
3.3 Uwezo wa Kupima na Kuchora Ramani kwa Teknolojia ya Kompyuta.
- Uchoraji wa ramani kwa kutumia mashine za photogmmmetry zilizoshikizwa na kompyuta
- Uingizaji wa ramani katika kompyuta kwa njia ya board or screen digitization hadi ukubwa wa AO
- Upimaji ardhi kwa kutumia kifaa cha Total Station ambacho hunasa vipimo na takwimu moja kwa moja katika mfumo wa kompyuta
- Upimaji kwa taaluma ya anga za juu GPS
- Kupata ramani ya umbile la ardhi kuonyesha mwinuko na mabonde usawa wa bahari
- Upimaji wa mwinuko wa barabara
- Usanifu wa ramani kwa kompyuta
UCHORAJI RAMANI KUTOKANA NA PICHA ZA ANGA
- Kuchapa ramani kutoka kwenye kompyuta katika rangi moja au nyingi
4. Teknolojia ya Kisasa
Kwa kutumia teknolojia ya kisasa, idara ina uwezo wa kuchora na kutoa ramani katika mfumo wa kompyuta. Ramani za baadhi ya maeneo hususan ya kati ya Jiji na Manispaa zote nchini ziko katika mfumo wa kompyuta. Ramani au Kumbukumbu Kuu ya Uoto wa Tanzania ipo katika mfumo wa kompyuta
5. Upatikanaji wa Bidhaa na Huduma za Idara.
5.1 Huduma za Upimaji na
Ramani
Bidhaa za kawaida zikiwemo ramani, picha za anga huuzwa katika duka la ramani lililopo jengo la Casino katika makutano ya barabara za Kivukoni Front na Luthuli, jijini Dar es Salaam
5.2 Bidhaa na huduma ya pekee hupatikana kwa maombi ya mteja.
Kwa maelezo zaidi, wasiliana na:
Mkurugenzi,
Idara ya Upimaji na Ramani
S.L.B. 9201, Dares Salaam
Simu: 255-22-2121894/2123735
Fax: 2138962/2123735
barua kipepe: smd@raha.com
1.0 Utangulizi
Lengo la upimaji wa ardhi ni kupata kielelezo halisi na cha kipekee cha utambulisho wa kipande cha ardhi hususan sehemu kilipo, umbile na ukubwa wake na uhusiano na mazingira yanayokizunguka. Hi mwananchi aweze kupewa hati ya kumiliki ardhi hakuna budi kuwa na kumbukumbu ya mipaka ya kipande cha ardhi husika. Upimaji wenye lengo hilo huitwa upimaji miliki (cadastral survey)
Ramani inayoonyesha viwanja baada ya upimaji kukamilika
2.0 Upimaji Miliki Mijini:
Maombi ya miliki yanawasilishwa kwa Afisa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya, Jiji, Manispaa au Mji husika. Afisa Ardhi atakagua eneo kuthibitisha kuwa:
- Ardhi husika ina mchoro wa mipangomji ulioidhishwa
- Ardhi husika ni huru, haina migogoro ya mipaka, miliki au hati iliyowekwa rehani
- Ardhi husika haina upimaji uliotangulia na kama upo haikusudiwi kuutumia kumilikisha ardhi hiyo. Afisa ardhi atafanya mawasiliano na Mpima ardhi wa Halmashauri husika kwa kujaza fomu SF 37 (request for survey) ikiambanishwa na mchoro wa mipangomiji ulioidhinishwa. Mpima Ardhi wa Halmashauri atatoa maelekezo ya Upimaji (Survey Instruction) kwa mpimaji.
Baada ya upimaji kukamilika, nyaraka zote za upimaji huwasilishwa kwa Mkurugenzi wa upimaji na Ramani kukaguliwa, kuthibitishwa na kusajiliwa kama kumbukumbu rasmi ya mipaka ya Ardhi husika.
Upimaji mijini huzingatia michoro ya Mipango miji na sio mipaka ya asili jinsi majirani wanavyokaa. Hapa ndipo umuhimu wa kuwa na ardhi huru unapojitokeza ili yeyote anayeathiriwa na utekelezaji wa mchoro wa mipango miji ashirikishwe kikamilifu ikiwa ni pamoja na kufidiwa kwa mujibu wa sheria.
Chini ya Sheria Sura Na. 390 (Sheria ya Upimaji Ardhi) plani ya upimaji iliyoidhinishwa ndio uthibitisho rasmi wa mipakaya ardhi iliyopimwa. Kutokana na hili hatua ya kuomba upimaji, utekelezaji wake, ukaguzi, uthibitishwaji na usajili wa plani lazima viwe makini kuepusha matatizo kama vile miliki kutolewa juu ya nyingine.
Upimaji wa ardhi kwa kutumia vifaa vya mawasiliano
ya masafa ya anga za juu (Satellite Global Positioning
System)
3.0 Upimaji Miliki Kijijini:
Maombi ya upimaji ardhi yanawasilishwa kwa Afisa Ardhi wa Halmashauri. Afisa Ardhi atachunguza na kuthibitisha yafuatayo:
- Ardhi iliyoombewa upimaji ni ya mhusika na kuwa ni huru na haina migogoro ya miliki au mipaka.
- Iwapo mhusika ni mwekezaji, kijiji kimetenga ardhi hiyo ili ihawilishwe kumilikishwa na kamishna wa ardhi.
- Kuna mihutasari ya vikao vya Halmashauri ya kijii vilivyopitisha / vilivyotenga Ardhi kwa mwekezaji.
- Vibali vya kumiliki ardhi kulingana na ukubwa wake vinapatikana katika ngazi ya Kijiji, Wilaya, Mkoa au Wizara.
Afisa Ardhi atawasiliana na Mpima wa Halmashauri kwa kujaza fomu SF 37 (Request for Survey) iliyoambatana na mchoro wa ardhi inayoombewa upimaji, nakala za mihutasari na vibari vya kumilikisha.
Upimaji unapokamilika, nyaraka zote huwasilishwa kwa Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kukaguliwa, kuthibitishwa na hatimaye kusajiliwa kama kumbukumbu rasmi ya mipaka ya ardhi iliyopimwa. Plani za hati (deed plan) huandaliwa kutokana na Plani za upimaji zilizothibitishwa.
Kwa maoni au maswali wasiliana na:
Mkurugenzi, Upimaji na Ramani
P.O. Box 9201,
Simu: +255-22-21373513894
Fax: +255-22-21237335138962
Kivukoni/Luthuli Road
Email:smd@raha.com
Tovuti: www.ardhi.go.tz